BK’
Sitaki Demu Remix
[Verse 1: B.K.]
B.K. ni ujio usio na ufagio 'pendo langu kwako sio
Nimemua wangu uamuzi sihiitaji tena makuzi
Wewe ki vyako 'sijali msamaha wako 'maneno yako, ng'ata ng'ata vidole vyako
Mimi sio wako kaa kitako, sikitikia umalaya wako
Si ulijali midako umbo lako hio sura yako
Ukajiona mipagawisho 'kumbe michosho
Pendo lako miyeyusho
Mimi nilibugi kwakweli wala sizugi
Sasa sihitaji demu
Mimi kijana timamu 'wala hunitii wazimu
Si ulisema nakula ndumu?, sasa ya nini kunighasi?
Akilini mwangu huna nafasi maneno haya naeleza
Wewe kwangu ulicheza 'hivyo sioni sababu kurudi kwa we usie na adabu, mwingi wa kutia ghadhabu 'unanata bila sababu we vipi?
Hivi utotoni hukuvishwa nepi?
Wewe unaona safi eh kila mmoja umdandie
Hii kwangu mi hapana labda wengine bila dhana
Nitakuaminiaje? na uwe nami ili iweje?

[Chorus: Juma Nature]
Walimwengu walikwisha niambia kuwa demu wangu mimi hafai (Hafai)
Mimi nikawabishia nikawaona wao kuwa ndio hawafai (Hawafai)
Hivi sasa mi najuta 'sitaki demu sihiitaji demu (Sitaki demu)
Bora nitafute mchumba (Sitaki demu)
Sihiitaji demu
[Verse 2: Juma Nature]
Kanuni ya kisanii ngoma ukweli una matter
Utaipata pata, pata, pata
Nna anza saga continue kisa kinaendelea
Nilipo ingia ndani ya gari nilimkuta msichana bonge hivi 'anaitwa Jacky "Samahani lakini si ku park eh?"
Akasema mi naomba twendeni ndani tukale
Halafu tukitoka hapa mm 'mkalale
Zikapita (?) mbili tulipendana sio siri
Mapenzi yaliiva yakawa yale ya kijasiri
Nikapata trip moja kwenda Tanga kusafiri
Niliporudi mama yangu magari
Leo Nissan Patrol kesho pick-up nyeupe inaendeshwa na yule bishoo
Nikimuuliza Oh, ugomvi 'Kaka yangu
Nikimuuliza ugomvi oh 'Baba yangu
We mtoto we! una muongopea nani hapa?
Wakati hapa mjini ukiwa nazo una (?)
Simu kila sekunde 'ya kazi moja mapenzi kumi
Tutaishi maisha ya (?) wakati deki ina kula kanda
Kumbe ulikuwa hujui kwasababu gani naitwa Qiblah
Napenda mvumilivu ila nikichoka naacha jumla
Visa vilianza siku ambayo nilikwenda hosteli
Kama saa nne na robo usiku na sekunde arobaini na nane hivi
Nikalikuta njemba moja linacheki TV
Kukawa kuna mademu wengine kama nane hivi
Sauti zao za uwizi bwana asikuambie mtu
Nikatoka zangu na kwenda kununua viepe
(?) kuuliza jamani hivi viepe mtashiba kweli?
Wakasema hivi viepe ni vingi sana kwa (?) yetu sisi, isitoshe hatuli sana nadhani nyie mnajulikana
Wamejaa uongo, ngenga na roho ya chuki tu 'wanakula hao
Mwanamke gani mkikorofishana hamuelewani?
Ana vi macho vidogo utamuona hata avae miwani
Na tabia yake mbaya afadhali hata ile shetani
Akuoe nani mimi? thubutu yako
Cha msingi tembea na bwana mmoja ukishindwa tumia Condom
[Chorus]
Walimwengu walikwisha niambia kuwa demu wangu mimi hafai (Hafai)
Mimi nikawabishia nikawaona wao kuwa ndio hawafai (Hawafai)
Hivi sasa mi najuta 'sitaki demu sihiitaji demu (Sitaki demu)
Bora nitafute mchumba (Sitaki demu)
Sihiitaji demu

[Hook]
Kipi kime kugusa we kisusa uliyosuswa
Mpaka ukaamua kuwaambia wenzio kuwa una nirusha, una nirusha?
Sitaki demu 'emu huko
Jamani
Kipi kime kugusa we kisusa uliyosuswa
Mpaka ukaamua kuwaambia wenzio kuwa una nirusha, una nirusha?
Sitaki demu 'emu huko
Jamani

[Chorus]
Walimwengu walikwisha niambia kuwa demu wangu mimi hafai (Hafai)
Mimi nikawabishia nikawaona wao kuwa ndio hawafai (Hawafai)
Hivi sasa mi najuta 'sitaki demu sihiitaji demu (Sitaki demu)
Bora nitafute mchumba (Sitaki demu)
Sihiitaji demu

(Instrumentals)